"

Albamu ya Video

Bilioni 9 kukamilisha miradi ya maji Kagera

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa jumla ya shilingi bilioni 9.7 kukamilisha miradi ya maji maeneo mbalimbali mkoani Kagera.

Imewekwa: Aug 15, 2020

Tatizo la maji Nyag’wale lapatiwa ufumbuzi

Naibu Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso ameagiza kufungwa kwa transformer kubwa ili mradi wa maji wa Nyang’wale uanze kufanya kazi. Agizo hilo amelitoa baada ya kikao kifupi na wataalamu wa Wizara ambao walibainisha kuwa transformer iliyofungwa haina uwezo wa kusukuma maji.

Imewekwa: Aug 15, 2020

Wizara yaokoa Bilioni 4 mradi wa Maji Sumbawanga

Naibu Waziri Wizara ya Maji, Mhe. Jumaa Aweso amewapongeza maafisa wa Wizara kwa kutekelezwa mradi wa maji wa Muze Group wilayani Sumbawanga na kuokoa zaidi ya Bilioni 4.

Imewekwa: Aug 10, 2020

Sasa mteja wa maji kupata huduma ndani ya sku Saba

Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso ameziagiza Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira kote nchini kuhakikisha wananawaunganishia wateja wapya ndani ya siku saba.

Imewekwa: Aug 10, 2020

Majisafi na Salama. Sasa ni zamu ya Mbalizi

Wakazi wa Mbalizi mkoani Mbeya wameanza kupata huduma ya majisafi na salama kufuatia utekelezaji wa mradi wa maji wa Mbalizi ambao umetekelezwa na Mamlaka ya majisafi na USafi wa Mazingira Mbeya. Mradi huo ni moja ya añadí alizozitoa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli

Imewekwa: Aug 10, 2020

Mbunge Kitwanga afurahishwa na kasi ya usambazaji maji nchini

Aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Misungwi Mkoani Mwanza (2015-2020) Mhe. Charles Kitwanga amefurahishwa na kasi ya usambazji maji nchini. Amesema amekuwa akitembelea Mamka za Maji ikiwemo ile inayosimamia usambazaji maji yanayotokea ziwa Victoria kwenda Mikoa ya Mwanza, Geita, Tabora na Shinyanga (KASHWASA) na kuridhishwa na Utendaji kazi wao.

Imewekwa: Jul 26, 2020