"

Albamu ya Video

UN yaikubali TZ usimamizi wa Rasilimali Maji na Usafi wa Mazingira

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Global Water Partinership Tanzania Dkt. Victor Kongo amesema Tanzania imefanya vizuri katika utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa ya Usimamizi endelevu wa Rasilimali za maji na Usafi wa Mazingira. Globala Water Partinership inafanya kazi kwa niaba ya Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia mazingira (UNEP)

Imewekwa: Sep 06, 2020

Bodi za Mabonde zakabidhiwa pikipiki

Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Anthony Sanga amekabidhi pikipiki 100 kwa Bodi za Mabonde ya Maji nchini na kuwataka wazitumie vizuri kukusanya mapato na kutunza vyanzo vya maji.

Imewekwa: Sep 06, 2020

Poland kupiga tafu miundombinu ya maji Dar na Dodoma

Leo Septemba 1, 2020 Maafisa wa Wizara ya Maji wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara Mhandisi Anthony Sanga wamekutana na ujumbe kutoka Ubalozi wa Poland kwa ajili ya majadiliano maalumu yaliyolenga ushirikiano baina ya nchi hizo mbili katika kuimarisha sekta ya maji kwa miji ya Dodoma na Dar es Salaam.

Imewekwa: Sep 04, 2020

Bilioni 40 kumaliza tatizo la maji Musoma

Naibu Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso ametembelea mradi wa maji wa Musoma ambao ujenzi wake unaendelea. Mradi huu ambao unatarajia kutumia zaidi ya bilioni 40 utawezesha maeneo mbalimbali ya mji wa musoma kuwa na ziada ya maji safi na salama.

Imewekwa: Aug 24, 2020

Aweso aagiza miradi ya maji Mwanza ikamilike haraka

Naibu Waziri wa Maji Mhe. Jumaa amewataka watalamu wa Wizara kuhakikisha miradi ya maji inayotekelezwa katika jiji la Mwanza inakamilishwa haraka.

Imewekwa: Aug 24, 2020

Huduma ya Majisafi yapiga hodi Rombo

Maafisa wa Wizara ya Maji wametembelea mradi wa maji Rombo na kuridhishwa na utekelezaji wake. Mradi huu unalenga kuongeza kiasi cha maji kwenye tanki linalohudumia makao makuu ya wilaya ya Rombo.

Imewekwa: Aug 24, 2020