"

Albamu ya Video

Zaidi ya wakazi 30,000 kunufaika na mradi wa maji wa Arri-Hasha Wilayani Mbulu

Wakazi wapatao 30,000 wanatarajia kunufaika na mradi wa maji wa Arri-Hasha unaotekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Babati (BAWASA) kwa thamani ya shilingi Bilioni 1.6. Mradi huu umefikia asilimia 80 ambapo vituo vya kuchochea maji 14 kati ya 52 vimeanza kutoa huduma

Imewekwa: Aug 24, 2020

Katibu Mkuu Maji ateta na Balozi wa Denmark miradi ya maji Tanzania

Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Anthony Sanga amekutana na kuzungumza Balozi wa Denmark nchini Tanzania, Mhe. Mette Dissing Spandet kuhusu ushirikiano baina ya nchi hizo kwenye Sekta ya Maji. Mazungumzo hayo ya awali yalilenga ufadhili wa utekelezaji wa ujenzi wa miradi ya maji hususan kwenye maeneo ya usambazaji wa majisafi na usafi wa mazingira kwenye majiji ya Dodoma na Dar es Salaam, kabla ya kukutana tena na kujadili masuala ya kiufundi katika kutekeleza miradi hiyo

Imewekwa: Aug 17, 2020

Miradi ya Force account imepunguza gharama na muda wa utekelezaji.

Utekelezaji wa miradi ya maji kwa kuwatumia wataalam wa Wizara imesaidia kuokoa muda, na kupunguza gharama. Pia imewezesha miradi hiyo kutekelezwa kwa kutumia vifaa vyenye ubora unaostahili

Imewekwa: Aug 15, 2020

Mamlaka za Maji kuweni wabunifu kutafuta fedha- Prof. Mbarawa

Waziri wa Maji Prof. Makame Mbarawa amezitaka Mamlaka za Maji kote nchini kuiga mfano wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Kahama ambao wametekeleza miradiya maji kwa kutumia fedha zao za ndani.

Imewekwa: Aug 15, 2020

Wateja wapya wa maji wapata ofa ya kulipa taratibu

Waziri wa Maji Prof. Makame Mbarawa amesikia kilio cha wananchi wa Mji wa Kahama na Kuiagiza Mamlaka ya Maji ya Mji huo kuhakikisha kila mwombaji anapatiwa huduma.

Imewekwa: Aug 15, 2020

Aweso atoa siku 30 kukamilisha mradi wa maji Kigoma

Naibu Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso ametoa siku 30 kukamilisha mradi wa maji Nyarubuye Kakonko Kigoma. Mradi huo unaotekelezwa kwa mfumo wa force account unategemea kutumia shilingi milioni 197 kutoka shilingi milioni 500 zilizopangwa iwapo ungekabidhiwa kwa

Imewekwa: Aug 15, 2020