Habari

Serikali Yajizatiti Kutunza Vyanzo vya Maji kwa Ustawi wa Taifa
Serikali kupitia Wizara ya Maji inaendelea kuongeza kasi ya juhudi za kutunza na kulinda vyanzo vya maji nchini, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuhakikisha usalama wa maji kwa matumizi ya sasa na kwa vizazi vijavyo.... Soma zaidi
Imewekwa: May 21, 2025

Kamati ya Bunge ya Bajeti Yapokea Taarifa ya Utekelezaji wa Mfuko wa Taifa wa Maji
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti imepokea taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Mfuko wa Taifa wa Maji kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko huo, Wakili Haji Nandule, katika kikao rasmi kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma.... Soma zaidi
Imewekwa: May 21, 2025

Sekta ya Maji Yazidi Kuimarika Kupitia Ushirikiano na Wadau wa Kimataifa
Wizara ya Maji imekutana na ujumbe kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) pamoja na Asasi ya Kimataifa ya WaterAid kwa lengo la kuimarisha ushirikiano katika maeneo ya maji, usafi wa mazingira na usafi binafsi.... Soma zaidi
Imewekwa: May 21, 2025

Tanzania na Ujerumani Kuendeleza Uhifadhi wa Maeneo Oevu ya Katuma
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Maji, kwa kushirikiana na Serikali ya Ujerumani kupitia Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ), zimesaini mkataba wa utekelezaji wa Mradi wa Uhifadhi wa Maeneo Oevu na Bioanuwai katika Kidakio cha Katuma, unaofahamika kama Mradi wa IKI Katuma.... Soma zaidi
Imewekwa: May 21, 2025

Miradi ya Maji Yaendelea Kutekelezwa Nchini-Waziri Mkuu
Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maji nchini ili kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma ya majisafi na salama katika maeneo yao ya makazi.... Soma zaidi
Imewekwa: May 19, 2025

Naibu Waziri Kundo Aongoza Ujumbe wa Tanzania Mkutano wa Mawaziri Wa Bonde la Ziwa Victoria Nchini Kenya
Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Mathew ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 23 wa Baraza la Mawaziri wa Kisekta wa Kamisheni ya Bonde la Ziwa Victoria (LVBC) Jijini Kisumu, nchini Kenya.... Soma zaidi
Imewekwa: May 19, 2025