Vitengo

Kitengo cha Uaandaji wa Miradi na Uratibu

Lengo

(i)Kuwezesha utayarishaji wa miradi na kuifanya iweze kupata fedha za utekelezaji kutoka taasisi za kifedha;

(ii)Kuratibu wadau wa maendeleo na ufutiliaji wa pamoja katika miradi ya sekta ya maji;

(iii)Kupitia maandiko ya mradi kutoka kwa Idara, Vitengo na Taasisi za Wizara na kuwasilisha kwa wadau wa maendeleo kwa ajili ya kutafuta fedha;

(iv)Kuratibu ufuatiliaji wa utekelezaji wa programu za sekta ya maji;

(v)Kuwezesha upatikanaji wa fursa kwa ajili ya kujenga uwezo kwa Wizara na Taasisi ili kuongeza ufanisi wa utekelezaji wa miradi;

(vi)Kukuza na kuwezesha ushiriki wa sekta binafsi katika sekta ya maji;

(vii)Kuratibu uandaaji wa viwango vya usanifu na usimamizi wa miradi ya maji na usafi wa mazingira;

(viii)Kuratibu sherehe za uzinduzi wa miradi kwa kushirikiana na Idara, Vitengo na Taasisi zinazotekeleza miradi; na

(ix)Kuwezesha utafutaji wa rasilimali fedha kwa ajili ya miradi ya maji na usafi wa mazingira kwa kushirikiana na Idara ya Sera na Mipango na Taasisi za Wizara..

Kitengo kinaongozwa na Mkurugenzi

Kitengo cha Fedha na Uhasibu

Lengo

Kufanya kazi ya menejimenti na utunzaji wa fedha.

Kitengo kinafanya kazi zifuatazo:-

Mshahara

(i) kuandaa na kufanya malipo ya mshahara kwa wakati ;

(ii) Menejimenti ya orodha ya malipo; na

(iii) Bajeti ya stahili

Ofisi ya Fedha

(i) Kuratibu masuala yote yanayohusu malipo.

Mapato

(i) Makusanyo ya mapato; na

(ii) Kuratibu ukusanyaji wa mapato.

Pensheni

(i) Kuandaa nyaraka za malipo kwa wakatition ; na

(ii) Kutunza kumbukumbu kuhusu pensheni.

Bajeti

(i) Kuandaa bajeti; na

(ii) Kufuatilia matumizi.

Ukaguzi

(i) Kupitia na kuhakikisha nyaraka za malipo zina viambatisho vinavyostahili kuendana na taratibu zilizopo;

(ii) Kupitia nyaraka za kifedha kama zimezingatia Sheria, Kanunia, Taratibu na Miongozo iliyopo; na

(iii) Kutoa mrejesho kuhusu hoja za kikaguzi.

Kitengo kinaongozwa na Mhasibu Mkuu.

Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani

Lengo

Kushauri na kuratibu matumizi bora ya rasilimali.

Kitengo kinafanya kazi zifuatazo:-

(i) Kukagua taarifa na rikodi za kifedha;

(ii) Kukagua taarifa ili kuhakikisha zimeandaliwa kwa kuzingatia taratibu na sheria za matumizi;

(iii) Kukagua na kupitia taarifa za akaunti za mapato na matumizi kuhakikisha taratibu zimezingatiwa;

(iv) Kuandaa taratibu za ukaguzi kwa mujibu wa viwango vya kimataifa;

(v) kukagua, kupitia na kuandaa ripoti za kifedha na ripoti nyingine;

(vi) Kupitia na kuandaa ripoti kuhusu mifumo ya utunzaji rasilimali na uhakiki wake;

(vii) Kupitia na kutoa ripoti kuhusu matokeo ya kazi / programu kama yanaendana na lengo/ malengo yalivyopangwa;

(viii) Kushauri na kusaidia katika utekelezaji wa maelekezo ya ripoti mbalimbali za kikaguzi;

(ix) Kukagua na kutoa taarifa kuhusu uthibiti na utoshelevu wa mifumo ya TEHAMA;

(x) Kuandaa na kutekeleza mkakati wa ukaguzi ; na

(xi) Kufanya ukaguzi wa utendaji katika miradi ya maendeleo.

Kitengo kinaongozwa na Mkaguzi Mkuu wa Ndani.

Kitengo cha Manunuzi

Lengo

Kutoa usaidizi na utaalam katika manunuzi ya vitu na huduma, utunzaji na usambazaji wa vifaa.

kitengo kinafanya kazi zifuatazo:-

(i) Kushauri masuala yanayohusu manunuzi ya vitu na huduma,pamoja na menejimenti yake;

(ii) Kusimamia na kuhakikisha taratibu za manunuzi zinafuatwa kwa kuzingatia Sheria ya Manunuzi;

(iii) Kuandaa mpango wa manunuzi kila mwaka;

(iv) Kununua, kutunza na kusimamia usambazaji wa vitu na huduma mbalimbali ;

(v) Kutunza daftari la manunuzi;

(vi) Kushiriki kama katibu wa Kamati ya Manunuzi ya Wizara kwa mujibu wa Sheria ya Manunuzi;

(vii) Kuweka viwango vya vitu na huduma zinazo nunuliwa na kufuatilia vina ubora wa thamani ya fedha ; na

(viii) Kuandaa bajeti na ripoti mbalimbali za Kitengo.

Kitengo kitaongozwa na Mkurugenzi.

Kitengo cha Huduma za Sheria

Lengo

Kutoa ushauri wa kisheria kwa wizara

Kitengo kinafanya kazi zifuatazo:-

(i) Kutoa ushauri kwa wizara na taasisi zake katika masuala yote ya kisheria;

(ii) Kushiriki katika kuandaa na kutoa usaidizi katika kuandaa masuala ya machapisho ya kisheria, na sheria kabla ya kuwasilisha kwa Mwanasheria Mkuu;

(iii) Kufuatilia na kujibu masuala ya kisheria Mahakamani na kutunza kumbukumbu za maamuzi ya Mahakama.

Kitengo kinaongozwa na Mkurugenzi.

Kitengo cha TEHAMA

Lengo

Kutoa ushauri na utaalam kuhusu masuala ya TEHAMA .

Kitengo kitafanya kazi zifuatazo:-

(i) Kutekelezaji wa sera ya TEHAMA na Serikali mtandao;

(ii) Kuunda na kuratibu mfumo shirikishi wa TEHAMA wa wizara;

(iii) Kutunza na kuhakikisha mifumo ya TEHAMA na vifaa vyake iko salama;

(iv) Kuratibu na kusaidia utaalamu katika ununuzi wa mifumo na vifaa vya TEHAMA;

(v) Kuanzisha na kuratibu matumizi ya barua pepe (za ndani na nje ya wizara); na

(vi) Kufanya utafiti na kushauri maeneo yanayoweza kutumia TEHAMA kama nyenzo ya kuongeza ubora katika utoaji huduma.

Kitengo kinaongozwa na Mtehama Mkuu.

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

Lengo

Kuratibu mawasiliano kati ya wizara na wadau wake

Kitengo kinafanya kazi zifuatazo:-

(i) Kuandaa machapisho ya elimu kwa umma kuhusu sera, programu na kazi mbalimbali zinazotekelezwa na wizara;

(ii) Kuratibu vyombo vya habari katika kazi za wizara;

(iii) Kuwashirikisha wananchi kwa kutoa taarifa pamoja na vyombo vya habari kuhusu masuala mbalimbali ya wizara;

(iv) Kutangaza kazi za wizara ;

(v) Kuratibu machapisho na mada kwa ajili ya mikutano na makongamano;

(vi) Kuratibu na kuandaa makala mbalimbali kuhusu wizara; na

(vii) Kuweka taarifa kila wakati katika tovuti ya wizara na mitandao ya kijamii.

Kitengo kinaongozwa na Afisa Habari Mkuu.

Kitengo cha Usimamizi wa Mazingira

Kitengo kinatekeleza majukumu yafuatayo;

i.Kuishauri Menejimenti ya Wizara kujumuisha katika sera, mipango na miradi ya maendeleo masuala yote yanayohusiana na hifadhi ya mazingira na kijamii;

ii.Kuratibu shughuli zote zinazohusiana na uhifadhi wa mazingira na kijamii katika sekta ya maji kwa kuzingatia sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004;

iii.Kuwa kiungo kati ya Wizara na Wizara/Taasisi zinazohusiana na masuala ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi kama vile Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira (VPO), Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na wadau wengine;

iv.Kuhakikisha kwamba masuala ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi yanajumuishwa katika Wizara, Idara, Vitengo na Taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Maji;

v.Kusimamia na kuratibu taratibu za utwaaji wa ardhi kwa ajili ya hifadhi ya vyanzo vya maji na ujenzi wa miundombinu ya miradi ya majisafi na usafi wa mazingira;

vi.Kuratibu utayarishaji wa taarifa ya Hali ya Mazingira ya Sekta ya Maji;

vii.Kuratibu na kuwezesha uandaaji wa taarifa za Tathmini za Athari kwa Mazingira (TAM), Ukaguzi wa Mazingira katika miradi na Tathmini ya Kimkakati ya Mazingira (Strategic Environmental Assessment) kwa kuzingatia Sheria ya Usimamizi wa Mazingira;

viii.Kuratibu na kuhakikisha afua za kuhimili athari za mabadiliko ya tabianchi zinazingatiwa na kujumuishwa katika mipango ya Sekta ya Maji.

Kitengo kitaongozwa na Afisa Mazingira Mkuu