Habari
WIZARA INAHITAJI WATUMISHI WENYE NIA YA MATOKEO
Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) amesema Wizara ya Maji inahitaji watumishi Wanaofanya kazi Kwa nia ya kuleta matokeo Ili kuimarisha huduma kwa wananchi.
Waziri Aweso ametoa kauli hiyo katika Mkutano wa Mwaka wa Wakala wa Maji safi na usafi wa Mazingira Vijijini (Ruwasa) pamoja na vyombo vya Watoaji Huduma ya Maji ngazi ya Jamii (CBWSOs) tukio lililofanyika katika ukumbi wa Jiji la Dodoma, Mtumba.
Ameitoa kauli hiyo wakati akizungumzia mchango mkubwa unaoendelea kutolewa na CBWSO's katika jamii.
Jumuiya hizo zinatambulika kisheria nchini hivyo zipo na jukumu kubwa la kuhakikisha maeneo korofi ya utolewaji huduma ya maji yanapata huduma hiyo.
Amewataka wadau hao kuendelea kuimarisha huduma kwa wananchi na kuendelea kuongeza nguvu katika utunzaji wa mazingira.
Waziri Aweso amesema Wizara ya Maji haitoendelea kulea watumishi wazembe wasio na nia ya kutoa matokeo chanya kwa wananchi.
Amesisitiza hatosita kuchukua hatua yoyote kwa watumishi wazembe Ili kuhakikisha lengo la serikali la huduma Bora kwa wakati wote linatimia kwa wananchi.
Kitengo cha Habari

