Habari
Wizara kutatua changamoto ya upatikanaji maji Karatu
Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Kundo Mathew (Mb) amesema Wizara inafanya taratibu za haraka kufikisha fedha katika Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Karatu ili kukamilisha miradi inayoendelea ambayo itawezesha huduma ya Maji katika mji huo kufikia asilimia 89.
Amesema hayo katika ziara ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb) wilayani hapo.
Amesema Wizara ya Maji inatambua changamoto ya huduma ya maji iliyopo katika mji huo ambapo kwa Sasa mji huo unapata huduma kwa asilimia 52.
Amesema kutokana na ukubwa wa changamoto hiyo Wizara imeendelea na utekekezaji wa miradi ambayo inahitaji takribani shilingi bilioni 2.5 hadi kukamilika.
Amesisitiza kuwa Serikali chini ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imewekeza fedha ya kutosha kuhakikisha kila mtanzania wakiwemo wananchi wa Karatu wanafikiwa na huduma ya Majisafi, Salama na ya kutosheleza.

