| |
| Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano |  |
Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kinaongozwa na Mchambuzi Mkuu wa Mifumo ya Kompyuta.
Kazi za Kitengo:
• Kusimamia utekelezaji wa sera ya Serikali Mtandao na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano katika Wizara.
• Kuhakikisha vifaa vya kompyuta na mtandao wa mawasiliano vinakuwa katika hali nzuri.
• Kusaidia na kutoa huduma za manunuzi ya vifaa vya kompyuta na Mtandao wa Mawasiliano katika Wizara.
• Kuanzisha na kusimamia matumizi ya mawasiliano ya baruapepe, mtandao wa ndani na nje ya Wizara.
• Kuratibu na kusimamia uanzishwaji wa mifumo ya kompyuta na benki za takwimu katika Wizara.
• Kuratibu na kusimamia uendelezaji wa watumishi katika matumizi ya Technolojia ya Habari na Mawasiliano (TEKNOHAMA).
• Kufanya tafiti zinazohusiana na utumiaji wa teknolojia ya mawasiliano kama chombo cha kuimarisha utendaji, utoaji wa taarifa muhimu na huduma kwa wananchi na wadau wote.
|
|
|
|