Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji 2006/2025 ilianza kutekelezwa mwaka 2006. Programu hii inatekelezwa nchi nzima (Tanzania Bara)
Madhumuni ya Programu ni:kutekeleza Sera ya Maji, kama ilivyofafanuliwa katika Mkakati wa Maendeleo wa Sekta ya Maji inatekeleza mipango inayolenga kuimarisha usimamizi wa raslimali za maji, kutoa huduma za maji na usafi wa mazingira na kutekeleza mipango kwa njia ya uwiano wa sekta nzima.
Programu ina programu ndogo nne ambazo ni:- Usimamizi wa Raslimali za Maji Uendelezaji wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini, Uendelezaji wa Majisafi na Uondoaji wa Majitaka Mijini, na Uimarishaji wa mfumo wa kitaasisi na kuzijengea uwezo.
Programu ndogo nne za WSDP (Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji)
1. Programu Ndogo ya Usimamizi wa Raslimali za Maji
2. Programu Ndogo ya Huduma ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Vijijini
3. Programu Ndogo ya Majisafi na Uondoaji wa Majitaka Mijini
4. Programu Ndogo ya Kujenga Uwezo wa Taasisi
Kwa maelezo zaidi kuhusu program Bonyeza hapa