| Dhima & Dira |  |
Dira
Dira ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji ni kuwa na mfumo endelevu wa kusimamia na kuendeleza rasilimali za maji utakaoleta manufaa ya kijamii na kiuchumi na kuimarisha sekta ya umwagiliaji kwa lengo la kuongeza uzalishaji, kuongeza pato la taifa na hivyo kuchangia katika kupunguza umaskini.
Dhamira
Dhamira ya Wizara ni kuhakikisha rasilimali za maji zinasimamiwa, zinaendelezwa na zinatumika kwa njia endelevu kwa kuwashirikisha wadau wote na kwa kuzingatia mahitaji ya sekta mbalimbali kupitia uboreshaji wa miundombinu ya usambazaji majisafi, uondoaji wa majitaka na kuwezesha mapinduzi ya sekta ya kilimo kutumia umwagiliaji kwa lengo la kuongeza uzalishaji na hivyo kuongeza kipato cha mwananchi.
|